Eda ni kipindi anachokaa mwanamke aliyeachika au aliyefiwa na mumewe, na baada ya kipindi hicho ndoa yake huwa halali. Na imeitwa eda kwa jina hili kutokana na jina la kiarabu ‘iddah’ kwa kukusanya kwake (idadi) ya miezi au ‘quruu’ [1] au hedhi au vipindi vya tohara ya hedhi.
HEKIMA YA KUHALALISHWA EDA
Hapa tunaona baadhi ya mawazo ya wanachuoni ambao wameona hizi ndizo hekima au sababu za kuwekewa eda shari'ah, ingawa hekima ya mwanzo na ya mwisho ni hiyo ya mwisho hapo chini ya fungu hili:
Kutambua kama mwanamke ni mjamzito au la.
Kuweza kubainika nasaba au kizazi ili kuepusha utata wa kutokujulikana nani ndiye baba.
Kipindi ambacho mke anakaa eda kiwe kifupi au kirefu kinaangaza mwangaza wa kweli kuhusu uzito wa ndoa yao na mkataba mtakatifu walioufunga baina yao.
Eda ya kufiwa inamwezesha mwanamke kutoa huzuni zake na kupata muda wa kujiliwaza na msiba uliomtokea wa kipenzi chake. Pia inamhifadhi kwa kutokuwa chombo cha kusemwa na kuzungumzwa kila apitapo.
Kupata nafasi mume na mke kutafakari kwa makini kuhusu mahusiano yao kabla hawajavunja muungano wao wa kifamilia na haswa katika talaqa ivunjikayo (ya kwanza au ya pili)
Ama HEKIMA ya juu kuliko zote kuhusu eda ni UTIIFU kwa maamrisho ya Mola wetu (Subhaanahu Wa Ta'ala). Kwani kuna wengi wanaotoa hoja za akilini mwao kama vile kudai kuwa siku hizi kuna utaalam wa kujua kama mwanamke ana mimba kwa vipimo bila haja ya kukaa eda mwanamke n.k. Hoja kama hiyo si ya busara maana ni sawa na kusema ‘siku hizi kuna kinga za mimba kama kondomu n.k, kwa hiyo zinaa iwe halali!’ Wamesahau kuwa HEKIMA kuu ni UTIIFU kwa Muumba na Utekelezaji wa MAAMRISHO yake na mengine ni ya ziada na wala si ya msingi. Allaah Anatujua zaidi kuliko tujijuavyo nafsi zetu.
HIVI UNAJUA NI KWA NINI MWANAMKE ANAKAA EDA ????
Eda ni kipindi anachokaa mwanamke aliyeachika au aliyefiwa na mumewe, na baada ya kipindi hicho ndoa yake huwa halali. Na imeitwa eda kwa jina hili kutokana na jina la kiarabu ‘iddah’ kwa kukusanya kwake (idadi) ya miezi au ‘quruu’ [1] au hedhi au vipindi vya tohara ya hedhi.
HEKIMA YA KUHALALISHWA EDA
Hapa tunaona baadhi ya mawazo ya wanachuoni ambao wameona hizi ndizo hekima au sababu za kuwekewa eda shari'ah, ingawa hekima ya mwanzo na ya mwisho ni hiyo ya mwisho hapo chini ya fungu hili:
Kutambua kama mwanamke ni mjamzito au la.
Kuweza kubainika nasaba au kizazi ili kuepusha utata wa kutokujulikana nani ndiye baba.
Kipindi ambacho mke anakaa eda kiwe kifupi au kirefu kinaangaza mwangaza wa kweli kuhusu uzito wa ndoa yao na mkataba mtakatifu walioufunga baina yao.
Eda ya kufiwa inamwezesha mwanamke kutoa huzuni zake na kupata muda wa kujiliwaza na msiba uliomtokea wa kipenzi chake. Pia inamhifadhi kwa kutokuwa chombo cha kusemwa na kuzungumzwa kila apitapo.
Kupata nafasi mume na mke kutafakari kwa makini kuhusu mahusiano yao kabla hawajavunja muungano wao wa kifamilia na haswa katika talaqa ivunjikayo (ya kwanza au ya pili)
Ama HEKIMA ya juu kuliko zote kuhusu eda ni UTIIFU kwa maamrisho ya Mola wetu (Subhaanahu Wa Ta'ala). Kwani kuna wengi wanaotoa hoja za akilini mwao kama vile kudai kuwa siku hizi kuna utaalam wa kujua kama mwanamke ana mimba kwa vipimo bila haja ya kukaa eda mwanamke n.k. Hoja kama hiyo si ya busara maana ni sawa na kusema ‘siku hizi kuna kinga za mimba kama kondomu n.k, kwa hiyo zinaa iwe halali!’ Wamesahau kuwa HEKIMA kuu ni UTIIFU kwa Muumba na Utekelezaji wa MAAMRISHO yake na mengine ni ya ziada na wala si ya msingi. Allaah Anatujua zaidi kuliko tujijuavyo nafsi zetu.
No comments