(75)
(اللّهُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ لاَ تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلاَ نَوْم...)
Mwenye
kusoma (Ayatul-Kursiy) pindi anapoamka atalindwa kutokana na majini
mpaka jioni, na atakaeisoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. (76)
(قُـلْ هُـوَ اللهُ أَحَـدٌ …)
(قُـلْ أَعـوذُ بِرَبِّ الفَلَـقِ…)
(قُـلْ أَعـوذُ بِرَبِّ النّـاسِ…)
(Mara tatu tatu)
(Mwenye kusisoma (sura hizi) mara tatu asubuhi na jioni zinamtosheleza na kila kitu.
(77)
أَصْـبَحْنا
وَأَصْـبَحَ المـلكُ لله وَالحَمدُ لله ، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا
شَريكَ لهُ، لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير ، رَبِّ
أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هَذا الْيَوْمِ وَخَـيرَ ما بَعْـدَهُ ،
وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ هَذا الْيَوْمِ وَشَرِّ ما بَعْـدَهُ ،
رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر ، رَبِّ أَعـوذُبِكَ
مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ وَعَـذابٍ في القَـبْر
“Tumeingia
wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Allaah , na sifa njema ni
zake Allaah , hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki, ila Allaah , hali
yakuwa peke yake, hana mshirika. Niwake Ufalme, na nizake sifa njema,
na yeye juu ya kila kitu ni muweza, Ee Mola, nakuomba kheri ya siku ya
leo, na kheri ya baada ya siku hii, na ninajilinda Kwako kutokana na
shari ya siku ya leo na shari ya baada ya siku hii. Ee Mola, najilinda
Kwako, kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee (uzee mbaya) Ee Mola
najilinda Kwako kutokana na adhabu ya moto na adhabu ya kaburi” (Na ikiingia jioni useme)
أَمْسَيْـنا
وَأَمْسـى المـلكُ لله وَالحَمدُ لله ، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا
شَريكَ لهُ، لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير ، رَبِّ
أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هـذهِ اللَّـيْلَةِ وَخَـيرَ ما بَعْـدَهـا ،
وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ هـذهِ اللَّـيْلةِ وَشَرِّ ما بَعْـدَهـا ،
رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر ، رَبِّ أَعـوذُبِكَ
مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ وَعَـذابٍ في القَـبْر .
(78)
اللّهُـمَّ بِكَ أَصْـبَحْنا وَبِكَ أَمْسَـينا ، وَبِكَ نَحْـيا وَبِكَ نَمـوتُ وَإِلَـيْكَ النِّـشور .
“Ee
Allaah kwa sababu yako tumeingia katika asubuhi, na kwa ajili yako
tumeingia jioni, na kwa ajili yako ndio tumekuwa hai, na kwa ajili yako
tutakufa, na kwako tutafuliwa”(Na ikifika jioni useme )
اللّهُـمَّ بِكَ أَمْسَـينا، وَبِكَ أَصْـبَحْنا، وَبِكَ نَحْـيا، وَبِكَ نَمـوتُ وَإِلَـيْكَ المَصـير
“Ee
Allaah kwa ajili yako tumefika jioni, na kwa ajili yako tumefika
asubuhi, na kwa ajili yako tuko hai na kwa ajili yako tutakufa na ni
kwako tu marejeo.(79)
اللّهـمَّ
أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك ،
وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت ، أَعـوذُبِكَ مِنْ
شَـرِّ ما صَنَـعْت ، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ
بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ .
“Ee
Allaah Wewe ni Mola wangu, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila
Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja wako, nami niko juu ya ahadi yako,
na agano lako, kiasi cha uwezo wangu, najilinda kwako kutokana na shari
ya nilicho kifanya, nakiri kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa
madhambi yangu, basi nakuomba unisamehe kwani hasamehe madhambi ila
Wewe”(80)
اللّهُـمَّ
إِنِّـي أَصْبَـحْتُ أَُشْـهِدُك ، وَأُشْـهِدُ حَمَلَـةَ عَـرْشِـك ،
وَمَلائِكَتِك ، وَجَمـيعَ خَلْـقِك ، أَنَّـكَ أَنْـتَ اللهُ لا إلهَ إلاّ
أَنْـتَ وَحْـدَكَ لا شَريكَ لَـك ، وَأَنَّ ُ مُحَمّـداً عَبْـدُكَ
وَرَسـولُـك .(أربع مرات حينَ يصْبِح أوْ يمسي)
“Ee
Allaah hakika mimi nimefika asubuhi nakushuhudia na nina washuhudia
wabeba wa arshi yako na malaika wako, na viumbe vyako vyote kwamba Wewe
ndiye Allaah hapana apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, hali ya kuwa
peke yako huna mshirika, na kwamba Muhammad ni mja wako na ni Mtume
wako”(Utasema hivi mara nne, asubuhi au jioni)
Atakaye yasema haya asubuhi au jioni mara nne Allaah سبحانه وتعالى atamuepusha na moto.
(81)
اللّهُـمَّ
ما أَصْبَـَحَ بي مِـنْ نِعْـمَةٍ أَو بِأَحَـدٍ مِـنْ خَلْـقِك ،
فَمِـنْكَ وَحْـدَكَ لا شريكَ لَـك ، فَلَـكَ الْحَمْـدُ وَلَـكَ الشُّكْـر
“Ee
Allaah sikuamka na neema yoyote au kati ya kiumbe chako chochote, na
neema ila inatoka kwako hali ya kuwa peke yako huna mshirika wako, ni
zako sifa njema na nizako shukurani” Atakae yasema haya kila asubuhi basi atakuwa ametekeleza shukurani ya siku nzima, na atakae yasema jioni atakuwa ametekeleza shukurani ya usiku mzima
(82)
اللّهُـمَّ
عافِـني في بَدَنـي ، اللّهُـمَّ عافِـني في سَمْـعي ، اللّهُـمَّ
عافِـني في بَصَـري ، لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ . (ثلاثاً)
اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكُـفر ، وَالفَـقْر ، وَأَعـوذُبِكَ مِنْ عَذابِ القَـبْر ، لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ . (ثلاثاً)
“Ee
Allaah nipe afya ya mwili wangu, Ee Allaah nipe afya ya usikizi wangu,
Ee Allaah nipe afya ya uwoni wangu,hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki
ila Wewe”(mara tatu )
“Ee Allaah hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri, na ufakiri, na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kaburi, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe” (mara tatu )
(83)
حَسْبِـيَ اللّهُ لا إلهَ إلاّ هُوَ عَلَـيهِ تَوَكَّـلتُ وَهُوَ رَبُّ العَرْشِ العَظـيم
“Allaah ananitosha, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Yeye, kwake Yeye nimetegemea, na Yeye ni Mola wa Arshi Tukufu” (mara saba asubuhi na jioni)
(84)
اللّهُـمَّ
إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في الدُّنْـيا وَالآخِـرَة ،
اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في ديني
وَدُنْـيايَ وَأهْـلي وَمالـي ، اللّهُـمَّ اسْتُـرْ عـوْراتي وَآمِـنْ
رَوْعاتـي ، اللّهُـمَّ احْفَظْـني مِن بَـينِ يَدَيَّ وَمِن خَلْفـي وَعَن
يَمـيني وَعَن شِمـالي ، وَمِن فَوْقـي ، وَأَعـوذُ بِعَظَمَـتِكَ أَن
أُغْـتالَ مِن تَحْتـي
“Ee
Allaah nakuomba msamaha na afya duniani na akhera. Ee Allaah hakika
mimi nakuomba msamaha na afya katika dini yangu na dunia yangu na jamaa
zangu, na mali yangu, Ee Allaah nisitiri uchi wangu, na unitulize khofu
yangu, Ee Allaah nihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kulia
kwangu, na kushoto kwangu, najuu yangu, na najilinda kwa utukufu wako
kwakutekwa chini yangu”(85)
اللّهُـمَّ
عالِـمَ الغَـيْبِ وَالشّـهادَةِ فاطِـرَ السّماواتِ وَالأرْضِ رَبَّ
كـلِّ شَـيءٍ وَمَليـكَه ، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْت ، أَعـوذُ
بِكَ مِن شَـرِّ نَفْسـي وَمِن شَـرِّ الشَّيْـطانِ وَشِـرْكِه ،
وَأَنْ أَقْتَـرِفَ عَلـى نَفْسـي سوءاً أَوْ أَجُـرَّهُ إِلـى مُسْـلِم .
“Ee
Allaah , Mjuzi wa yaliyofichika na yaliyowazi, muumba wa mbingu na
ardhi, Mola wa kila kitu, na Mfalme wake, nakiri kwamba hapana mola
apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, najilinda kwako kutokana na shari
ya nafsi yangu na shari ya shetani na shirki yake na kujichumia uovu kwa
nafsi yangu au kumletea Muislamu”(86)
بِسـمِ اللهِ الذي لا يَضُـرُّ مَعَ اسمِـهِ شَيءٌ في الأرْضِ وَلا في السّمـاءِ وَهـوَ السّمـيعُ العَلـيم (ثلاثاً)
“Kwa jina la Allaah ambae hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilicho ardhini, wala mbinguni, nae ni Msikivu na ni Mjuzi"(mara tatu )
(87)
رَضيـتُ بِاللهِ رَبَّـاً وَبِالإسْلامِ ديـناً وَبِمُحَـمَّدٍ صََلى الله عليه وسلم نَبِيّـاً . (ثلاثاً)
“Nimeridhika kuwa Allaah ndie Mola wangu, na Uislamu ndio dini yangu, na Muhammad صََلى الله عليه وسلم kuwa ni Mtume wangu”(mara tatu)
(88)
يا حَـيُّ يا قَيّـومُ بِـرَحْمَـتِكِ أَسْتَـغـيث ، أَصْلِـحْ لي شَـأْنـي كُلَّـه ، وَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـين
“Ewe
Uliyehai, Uliyesimama kwa dhati yako, kwa rehema zako ninakuomba
uniokoe, nitengenezee mambo yangu yote, wala usiniachie mambo yangu
mwenyewe (pasina kunisaidia) hata kwa muda (mdogo kama muda) wa kupepesa
jicho”(89)
أَصْبَـحْـنا
وَأَصْبَـحْ المُـلكُ للهِ رَبِّ العـالَمـين ، اللّهُـمَّ إِنِّـي
أسْـأَلُـكَ خَـيْرَ هـذا الـيَوْم ، فَـتْحَهُ ، وَنَصْـرَهُ ، وَنـورَهُ
وَبَـرَكَتَـهُ ، وَهُـداهُ ، وَأَعـوذُ بِـكَ مِـنْ شَـرِّ ما فـيهِ
وَشَـرِّ ما بَعْـدَه .
“Tumeingia
asubuhi na imefika asubuhi na Ufalme ni wa Allaah, Mola wa viumbe
vyote, Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya siku hii ya leo,
ufunguzi wake na nusura yake, na nuru yake na baraka yake, na uongofu
wake, na najilinda kwako kutokana na shari ya kilicho ndani ya siku
hii, na shari ya baada ya siku hii”(Na ikiingia jioni useme)
أَمْسَيْـنا
وَأَمْسـى المُـلكُ للهِ رَبِّ العـالَمـين ، اللّهُـمَّ إِنِّـي
أسْـأَلُـكَ خَـيْرَ هـذهِ اللَّـيْلَة ، فَتْحَهـا ، وَنَصْـرَهـا ،
وَنـورَهـا وَبَـرَكَتَـهـا ، وَهُـداهـا ، وَأَعـوذُ بِـكَ مِـنْ شَـرِّ
ما فـيهـاِ وَشَـرِّ ما بَعْـدَهـا .
“Tumeingia
jioni na imefika jioni na Ufalme ni wa Allaah, Mola wa viumbe vyote,
Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya usiku huu, ufunguzi wake na
nusura yake, na nuru yake na baraka yake, na uongofu wake, na najilinda
kwako kutokana na shari ya kilicho ndani ya usiku huu, na shari ya
baada ya usiku huu”(90)
أَصْـبَحْنا
علـى فِطْـرَةِ الإسْلام ، وَعَلـى كَلِـمَةِ الإخْـلاص ، وَعلـى دينِ
نَبِـيِّنا مُحَـمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم وَعَاـى مِلَّـةِ
أبينـا إِبْـراهيـمَ حَنيـفاً مُسْلِـماً وَمـا كـانَ مِنَ المُشـرِكيـن .
“Tumeingia asubuhi na maumbile ya kiislamu na neno la ikhlasi na dini ya Mtume wetu Muhammad صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم na mila (dini) ya baba yetu Ibraahiym iliyo sawa hali yakuwa musilamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Allaah"(Na ikiingia jioni useme)
أَمْسَيْنا
علـى فِطْـرَةِ الإسْلام ، وَعَلـى كَلِـمَةِ الإخْـلاص ، وَعلـى دينِ
نَبِـيِّنا مُحَـمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم وَعَاـى مِلَّـةِ
أبينـا إِبْـراهيـمَ حَنيـفاً مُسْلِـماً وَمـا كـانَ مِنَ المُشـرِكيـن
“Tumeingia jioni na maumbile ya kiislamu na neno la ikhlasi na dini ya Mtume wetu Muhammad صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم na mila (dini) ya baba yetu Ibraahiym iliyo sawa hali yakuwa musilamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Allaah “(91)
سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ
“Ametakasika Allaah na sifa njema zote nizake” (mara mia moja)
(92)
لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير
“Hapana
mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Allaah peke yake, hana mshirika
wake, niwake Ufalme, na nizake sifa njema zote na Yeye juu ya kila kitu
ni Muweza”(mara kumi, au mara moja ukisikia uvivu)
(93)
Amesema Mtume صلى الله عليه وسلم “Mwenye kusema inapoingia asubuhi
لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير
“Hapana
mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Allaah peke yake hana mshirika
wake, niwake Ufalme na nizake sifa njema zote, na Yeye juu ya kila kitu
ni Muweza” ...kwa siku mara mia, basi ana thawabu za kuwaacha huru watumwa kumi na ataandikwa thawabu mia moja na atafutiwa madhambi mia moja, na atakuwa na kinga ya shetani kwa siku hiyo yote hadi jioni na hatakuwa mtu yeyote mbora kumshinda ila yule aliyefanya zaidi yake”
(94)
سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ عَدَدَ خَلْـقِه ، وَرِضـا نَفْسِـه ، وَزِنََـةَ عَـرْشِـه ، وَمِـدادَ كَلِمـاتِـه
“Ametakasika
Allaah na sifa njema zote ni zake, kwa hisabu ya viumbe vyake, na
radhi yake, na uzito wa arshi yake, na wino wa maneno yake “(mara tatu kila asubuhi )
(95)
اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ عِلْمـاً نافِعـاً وَرِزْقـاً طَيِّـباً ، وَعَمَـلاً مُتَقَـبَّلاً
“Ee Allaah, nakuomba elimu yenye kunufaisha, na riziki iliyo nzuri, na ibada yenye kukubaliwa”(96)
أَسْتَغْفِرُ الَّلهَ وَ أَتُوبُ إِلَيْهِ
“Namuomba msamaha Allaah na ninarejea Kwake” (mara mia kwa siku )
(97)
Alikuwa Mtume صلى الله عليه وسلم akisema asubhuhi na jioni :
أَعُوْذُ بِكَلِماتِ اللَّهِ التَّامَّتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ
“Najilinda na maneno ya Allaah yaliyotimia kutokana na shari aliyoiumba”(mara tatu jioni)
Mwenye kuisema jioni mara tatu hatodhuriwa na mdudu wa sumu (kama nyoka au kitumbo-ng'e) usiku huo .
(98)
اللّهُـمَّ صَلِّ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه، كَمـا صَلَّيْـتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم . وَبارِكْ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه، كَمـا بارِكْتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم . إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد
“Ee
Allaah mrehemu Muhammad, na wake zake, na kizazi chake, kama
ulivyowarehemu jamaa wa Ibraahiym. Na mbariki Muhammad, na wake zake,
na kizazi chake, kama ulivyowabariki jamaa zake Ibraahiym, hakika Wewe
Umesifika na Umetukuka”"Mwenye kuniombea rehema asubuhi mara kumi na jioni mara kumi, nitamuombea shifaa (msamaha) siku ya Qiyaamah"

No comments