Assalam alaikum
Hii ndio hadithi ninayotaka kujuwa usahihi wake na kama
ni sahihi ukiunganisha na ya Abuu Umama itakuwa ni shaihi kuomba dua
kwa pamoja baada ya swala ya fardhi? Kwani imethibiti dua ya pamoja na
pia imethibiti dua baada ya swala. Yaani moja ya sehemu inayo kubalika
dua ni baada ya swala ya faradh na kama
alivyosema imamu Tirmidhy (Allah amrehemu) kuwa ni hadithi hasan. Je?
hadithi hii inafaa kuwa ni hoja madhubuti kwamba kuomba dua baada ya
swala ya fardh ni sunnah na imethibiti kwa mtume Swalla llah alaih wa
sallam na ni muhimu sana kwa mtu kuomba dua baada ya swala ya fardhi
kwani ni moja ya sehemu inayokubaliwa dua
MAELEZO MENGINE YA MUULIZAJI KUHUSIANA NA SWALI LAKE
Assalam alaikum,
Hadithi ya Abuu Umama niloisema yazungumzia dua baada ya swala ni hii hapa kama
alivyo inukuu Imamu Shaukani ktk Nailu L’autwar. Pia hadithi hii
inapatikana ktk Riyadha swallihina hadithi ya 1,500. Pia nime attach
hadithi nilo andika kwa mkono, hii nimeikuta ktk vitabu hivi vya dua
vidovidogo, sijaiona ktk vitabu vya hadithi, nimeikopi pamoja na
muhtasari wa takhrij yake,sina hakika na usahihi wa hadithi hii
1. Swali la kwanza, naomba mnifahamishwe usahihi wa hadithi nilo andika kwa mkono (attachment number one) ama umadhubuti wake kama inafaa kufanyia kazi
2. Maelezo
kwa ufupi: Hadithi ya Abuu Umama; Ibn Hajar ktk Fathu lbar juzu ya 11
ukurasa 153 (toleo la mwaka 2003) Kitabu dda’awa (dua’u ba’ada swalat)
ameinukuu na akaunganisha na hadithi ya Twabari kutoka kwa jaafar
isemayo” dua baada ya swala ya Fardh ni bora kuliko dua baada ya swala
ya sunnat kama ilivyo kuwa ubora wa swala ya fardh kwa swala ya sunnat”
pia akanukuu manenoya Watu wa Hanbal kuhusu kauli ya Ibn Lqaiym ktk
kitabu chake cha Zadu l’ma’aad (alipo sema hakuna hadithi sahihi inayo
thibitisha dua baada ya swala)
3. Swali
la pili, Ikiwa hadithi ya Abuu Umama na maelezo ya Ibn Hajar na hadith
ya Twabari ni sahihi; Je kuomba dua baada ya swala ya Fardh ni Sunnat?
4. Swali
la tatu, ikiwa hadithi nilo andika kwa mkono (Swali la kwanza) ni
sahihi ama ni madhubuti na inafaa kufanyia kazi, na kwa kuwa baada ya
swala kuna kundi la watu, hivyo wakaamuwa miongoni mwao mmoja aombe dua
na wengine waitikie wakaifanyia kazi hadithi (kwani ni sababu ya
kujibiwa dua kama haidthi inavyo jieleza) na kwa kuwa kuomba dua baada
ya swala ni sahihi ikiwa Swali la pili yaani hadithi ya Abuu Umama ni
madhubuti, Je, kuomba dua kwa pamoja baada ya swala( yaani kufanyia kazi
hadithi nilo andika kwa mkono na ya Abuu Umama kwa pamoja) itakuwa ni
sunnat ama bid’a( ukizingatia sunnah inaweza kuwa Mtume Swalla llahu
alaihi wa sallam amesema(sio lazima afanye), ama amefanya, amekubali
jambo moja ktk ya haya matatu yaweza kuwa sunnat)
Wabillah taufiq
No comments