Header Ads

Cup of coffee on saucer

KIONGOZI WA BOKO HARAM ABUBAKAR SHEKAU AIBUKA KUKANUSHA KUUAWA KWAKE

Abubakar Shekau, kiongozi wa wanamgambo wa Boko haramu Nijeria amejitokeza na kukana uvumi kuwa alikuwa ameuawa.

Madai ya kufariki kwa Shekau yalianzishwa na raisi wa Chad Idriss Deby.
 Shekau alijirikodi na kusambaza katika vyombo vya habari.
Idara ya upelelezi nchini Nijeria yenye  utaalamu  ilichunguza rikodi ya Shekau na wakathibitisha kwamba sauti hiyo  bila shaka ilikuwa ya Shekau.

Mwaka 2014 raisi wa Chad alikuwa akikutana na wanamgambo wa Boko haram kwa lengo la kuleta amani baina yao na serikali ya Nijeria.

Majuma mawili yaliopita, serikali ya Chad ilidai kuwaua wanamgambo 117 wa Boko haram katika visiwa vya ziwa la Chad.

Boko haramu wamewaua zaidi ya watu 600 nchini Nijeria chini ya uongozi wa raisi Muhammadu Buhari.

No comments